Nyumbani Jumuiya Kwa kifupi Historia Matata Namna ya kusaidia Kujitolea Wenzi Picha Wasiliana nasi

 


KIBERA: HISTORIA


Mtaa wa mabanda wa Kibera ulianzishwa mwaka 1912, wakati serikali ya ukoloni wa uingereza ilipowapa makaazi  askari wa jamii ya wa nubi, walio na asili ya kutoka  sudan, Wanubi hawa walikuwa askari wa jeshi la mfalme wa uingereza katika nchi za afrika – yaani Kings of African Rifles.
(http://en.wikipedia.org/wiki/King%27s_African_Rifles)
Nyakati hizo eneo la Kibera lilikuwa msitu mkubwa ndipo wanubi hao wakaita eneo hilo Kibra ambalo kwa lugha ya kinubi inamaanisha msitu. Eneo hili hatimaye lilikuja kujulikana Kibera kutokana na matamshi ya ndimi mbali mbali. Mwaka 1918, serikali
ya kikoloni ilifanyia usorovyea eneo la Kibera likiwa maskani za askari wa asili ya kinubi na familia zao. Zama hizo eneo la Kibera lilikuwa msitu wa hekta 4,000 na ulikuwa na wanubi 600 tu.

Miaka 10 baadaye, 1928 Jeshi la uingereza lilitoa usamamizi wa mtaa huu kuwa baraza la jiji la Nairobi zama hizo, kauli ambayo ililazimishwa kufutwa kwa nyaraka miliki zote na wakazi wa mtaa huu wakamalizika kutoa stakabadhi za kudhibitisha kwamba wao ni wa asili ya Kinubi. Wanubi hao walitangazwa kuwa maskwota wa serikali ya ukoloni.
Kauli hii ilikuwa na maana kwamba kamishna wa Ardhi alikuwa na uwezo wa kufuta haki ya wa Nubi hao kuwa maswokta katika enelo hilo. Ni kutokana na sababu hii kwamba mijengo yote katika mtaa huu ilikuwa ya muda kwani serikali ilibakia na haki ya kuibomoa wakati wowote na kuitumuia ardhi hiyo kujenga miradi mingine.

Mwaka wa 1948 kulitokea mvuto wa kwanza wa kutaka kuwatimua wakaazi wa mtaa wa Kibera kutokana na msukumo wamatatizo ya kiafya. Licha ya athari za kiafya na ushafuzi wa mazingira, mtaa wa KIbera uliendelea kupanuka na hadi kufikia miaka ya 1970. Idadi ya wakaazi wa mtaa huu ulindelea kuongezeka kwa haraka na mwaka 1980, ulifisika kuwa na idadi kukwa ya watu waliokisiwa kuwa zaidi ya elfu 62,000 kutoka elfu 6,000 tu walikuwepo mwana wa 1965.
Mwaka 1992, mtaa huu ulikuwa naidadi ya watu waliokisiwa kuwa kati ya 248,360 na nusu millioni kufika mwaka 1998. Kulingana na takwimu za hesabu ya watu, mtaa hii ulikuwa unakua kwa asilimia 17 kwa kila mwaka. Suala hili liliekea kuwa kuende mtaa huu ukawa a idadi  kati ya watu 700,000 namilioni moja, kukiwa na  watu elfu mbili katika kila hekta moja na kati ya watu 3.2 na 4.6 kwa kila chumba kimoja, na hvyo kuufanya mtaa wa Kibera kuwa mkubwa zaidi barani Africa.

Mfumuko wa watu kuhamia mijini wakitokea vijijini umechangia pakubwa kuongezeka kwa idadi ya watu katika mtaa huu. Suala hilo limechangiwa na dhana kwamba jiji la Nairobi likiwa makao makuu ya serikalo, ndipo kuna nafasi nyingi za ajira. Ongeseko la watu  katika  mtaa wa Kibera, amabako kupangisha chumba ni rahisi kuliko sehemu nyingine yoyote ile jijini, kumechangiwa na kupungua  kwa uzalishaji wa mazao ya kilimo na ongezeko la idadi ya watu nchini.