Nyumbani Jumuiya Kwa kifupi Historia Matata Namna ya kusaidia Kujitolea Wenzi Picha Wasiliana nasi

 

 

Mtaa wa Kiber upo katika ardihi ya Serikali, unafahamika kama maskani haramuna huwezi kufikiriwa wakati wa kupanga mikakati na maendeleo jiji la Nairobi. Mtaa wa Kibera upo kilomita 7 kutoka kati mwa jiji la Nairobi.

Vijiji hivi vyote vinakumbana na matatizo sugu ya afya, kijamii, kiuchumi na mazingira. Nyumba za Kibera hujengwa vivi-hivi na kuwa  haziachi  nafasi. Katika  mtaa huu ni michache  na wakaazi wake hawana anwani na ni wachachwe waliofungulia masanduku ya barua.

Nyumba za mtaa huu ni za matope na ndani yake huwa na vyumba vingi vidogo – vidogo huku  zikiezekwa  kwa mabati ama debe. Nyumba nyingi za mtaa huu hazina veranda, kuta zake hazipo laini huku barabara zikiwa suala  nyeti hususan wakati mtu anapougua kwa haraka. Mianya iliyopo ni vichochoro ambavyo havi pitiki kwa gari. Wakati wa mioto magari hayawezi kufikia sehemu inayoungua. Mifereji michafu iliyo wazi ni jambo la kawaida katika mtaa huu.Tukataka na maji machafu vyote vinatupwa katika mitaro ya mifereji hii. Na wakati takataka hii inapokuwa rundo basi mitaro hiyo huwa imefungwa. Kwa sababu mtaa huu ni sehemu wanakoishi walalao – hio mitaro hii haipo mbali na nyumba  nyingi, ndiko mbu wanaosababisha  maradhi kibao wanakozaliana.
Licha ya matatizo ya kutokuwa na mitaro ya kuzoa maji taka, wakaati wa Kibera wanakumbana na matatizo mengi likiwepo la uhaba wa safi, elimu, matibabbu na stima. Isitoshe, wakaazi wa mtaa huu wanajikunyata peupe kwa sababu nyumba zao ni za  muda tu.

Na mwisho, idadi kubwa ya watu wanao athirikia kutokana na janga la Ukimwi ni  tatizo nyeti Takwimu zimebainisha kwamba zaidi ya  asilimia 15 ya wakaazi wa mtaa huu wameambukizwa viini vya HIV ama Ukimwi kamili. Idadi hii inaweza kuwa zaidi kwa sabu wengi wao ni watoto wa umri   wamiaka  mmoja  na pengine hawajapima damu. Waathiriwa wengi ni vijana, wazazi na watoto wachanga. Familia nyingi huwa na tatizo kubwa kwa sababu watoto hawa huchangia pakuwabwa kudhoofika kwa afya za  wazazi wao huku wao wenyewe wakiiwa hawana usewo wa kujifanya lolote. Wengi wa watoto hawa wameambukizwa viini  hivi, lakini sawia na wazazi wao, hawapati huduma zozote na matibabu wala dawa za kukubaliakana na magonjwa nyemelezi na  Kurefusha  maisha ya  waathiriwa.

Ni kutokana na matatizo haya kwamba vijana wa mtaa huu waliungana kubuni SHOFCO kama nguzo imara angalao wakabiliane  na baadhi ya matatizo kwa pamoja.

© 2006-2007 Shofco.org